17. kwa sababu alikuwa amehesabiwa pamoja na sisi, akapata sehemu ya huduma hii.
18. (Basi mtu huyu alinunua konde kwa ijara ya udhalimu; akaanguka kwa kasi akapasuka matumbo yake yote yakatoka.
19. Ikajulikana na watu wote wakaao Yerusalemu; hata konde lile likaitwa kwa lugha yao Akeldama, maana yake, konde la damu.)
20. Kwa maana imeandikwa katika chuo cha Zaburi,Kikao chake na kiwe ukiwa,Wala asiwepo mtu mwenye kukaa humo;tena,Usimamizi wake autwae mwingine.