51. Alipofika nyumbani hakuacha mtu kuingia pamoja naye ila Petro, na Yohana, na Yakobo, na babaye yule mtoto na mamaye.
52. Na watu wote walikuwa wakilia na kumwombolezea; akasema, Msilie, hakufa huyu, bali amelala usingizi tu.
53. Wakamcheka sana, maana walijua ya kuwa amekwisha kufa.
54. Akamshika mkono, akapaza sauti, akisema Kijana, inuka.
55. Roho yake ikamrejea, naye mara hiyo akasimama. Akaamuru apewe chakula.
56. Wazazi wake wakastaajabu sana, lakini akawakataza wasimwambie mtu lililotukia.