Lk. 8:3-11 Swahili Union Version (SUV)

3. na Yoana mkewe Kuza, wakili wake Herode, na Susana, na wengine wengi, waliokuwa wakimhudumia kwa mali zao.

4. Mkutano mkuu ulipokutanika, na wale waliotoka kila mji wakimjia, alisema kwa mfano;

5. Mpanzi alitoka kwenda kupanda mbegu zake; naye alipokuwa akizipanda, nyingine zilianguka karibu na njia, zikakanyagwa, ndege wa angani wakazila.

6. Nyingine zikaanguka penye mwamba; zilipoanza kumea zikakauka kwa kukosa rutuba.

7. Nyingine zikaanguka kati ya miiba, na miiba ikamea pamoja nazo ikazisonga.

8. Nyingine zikaanguka penye udongo mzuri; zikamea, zikazaa moja kwa mia. Alipokuwa akinena hayo alipaza sauti akisema, Mwenye masikio ya kusikilia, na asikie.

9. Wanafunzi wake wakamwuliza, Maana yake nini mfano huo?

10. Akasema, Ninyi mmepewa kuzijua siri za ufalme wa Mungu; bali wengine kwa mifano, ili wakiona wasione, na wakisikia wasielewe.

11. Na huo mfano, maana yake ni hii; Mbegu ni neno la Mungu.

Lk. 8