Lk. 7:45-50 Swahili Union Version (SUV)

45. Wewe hukunibusu; lakini huyu tangu nilipoingia hakuacha kunibusu sana miguu yangu.

46. Hukunipaka kichwa changu mafuta; bali huyu amenipaka miguu yangu marhamu.

47. Kwa ajili ya hayo nakuambia, Amesamehewa dhambi zake ambazo ni nyingi, kwa kuwa amependa sana; lakini asamehewaye kidogo, huyo hupenda kidogo.

48. Kisha alimwambia mwanamke, Umesamehewa dhambi zako.

49. Ndipo wale walioketi chakulani pamoja naye walianza kusema mioyoni mwao, Ni nani huyu hata asamehe dhambi?

50. Akamwambia yule mwanamke, Imani yako imekuokoa, enenda zako kwa amani.

Lk. 7