Lk. 6:27-32 Swahili Union Version (SUV)

27. Lakini nawaambia ninyi mnaosikia, Wapendeni adui zenu, watendeeni mema wale ambao wawachukia ninyi,

28. wabarikieni wale ambao wawalaani ninyi, waombeeni wale ambao wawaonea ninyi.

29. Akupigaye shavu moja, mgeuzie la pili, naye akunyang’anyaye joho yako, usimzuilie na kanzu.

30. Mpe kila akuombaye, na akunyang’anyaye vitu vyako, usitake akurudishie.

31. Na kama mnavyotaka watu wawatendee ninyi, watendeeni vivyo hivyo.

32. Maana mkiwapenda wale wawapendao ninyi, mwaonyesha fadhili gani? Kwa kuwa hata wenye dhambi huwapenda wale wawapendao.

Lk. 6