11. na ya kwamba,Mikononi mwao watakuchukua,Usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.
12. Yesu akajibu akamwambia, Imenenwa, Usimjaribu Bwana Mungu wako.
13. Basi alipomaliza kila jaribu, Ibilisi akamwacha akaenda zake kwa muda.
14. Yesu akarudi kwa nguvu za Roho, akenda Galilaya; habari zake zikaenea katika nchi zote za kandokando.