17. ambaye pepeo lake li mkononi mwake, naye atausafisha sana uwanda wake, na kuikusanya ngano ghalani mwake, bali makapi atayateketeza kwa moto usiozimika.
18. Basi, kwa maonyo mengine mengi aliwahubiri watu.
19. Lakini mfalme Herode alipokaripiwa na yeye kwa ajili ya Herodia, mke wa nduguye, na maovu yote aliyoyafanya Herode,
20. aliongeza na hili juu ya yote, alimfunga Yohana gerezani.
21. Ikawa, watu wote walipokwisha kubatizwa, na Yesu naye amebatizwa, naye anaomba, mbingu zilifunuka;
22. Roho Mtakatifu akashuka juu yake kwa mfano wa kiwiliwili, kama hua; sauti ikatoka mbinguni, Wewe ndiwe Mwanangu, mpendwa wangu; nimependezwa nawe.
23. Na Yesu mwenyewe, alipoanza kufundisha, alikuwa amepata umri wake kama miaka thelathini, akidhaniwa kuwa ni mwana wa Yusufu, wa Eli,
24. wa Mathati, wa Lawi, wa Melki, wa Yana, wa Yusufu,
25. wa Matathia, wa Amosi, wa Nahumu, wa Esli, wa Nagai,
26. wa Maathi, wa Matathia, wa Semei, wa Yusufu, wa Yuda,
27. wa Yoana, wa Resa, wa Zerubabeli, wa Shealtieli, wa Neri,
28. wa Melki, wa Adi, wa Kosamu, wa Elmadamu, wa Eri,
29. wa Yoshua, wa Eliezeri, wa Yorimu, wa Mathati, wa Lawi,
30. wa Simeoni, wa Yuda, wa Yusufu, wa Yonamu, wa Eliakimu,
31. wa Melea, wa Mena, wa Matatha, wa Nathani, wa Daudi,