Lk. 24:48-53 Swahili Union Version (SUV)

48. Nanyi ndinyi mashahidi wa mambo haya.

49. Na tazama, nawaletea juu yenu ahadi ya Baba yangu; lakini kaeni humu mjini, hata mvikwe uwezo utokao juu.

50. Akawaongoza mpaka Bethania, akainua mikono yake akawabariki.

51. Ikawa katika kuwabariki, alijitenga nao; akachukuliwa juu mbinguni.

52. Wakamwabudu; kisha wakarudi Yerusalemu wenye furaha kuu.

53. Nao walikuwa daima ndani ya hekalu, wakimsifu Mungu.

Lk. 24