1. Hata siku ya kwanza ya juma, ilipoanza kupambazuka, walikwenda kaburini, wakiyaleta manukato waliyoweka tayari.
2. Wakalikuta lile jiwe limevingirishwa mbali na kaburi,
3. Wakaingia, wasiuone mwili wa Bwana Yesu.
4. Ikawa walipokuwa wakifadhaika kwa ajili ya neno hilo, tazama, watu wawili walisimama karibu nao, wamevaa nguo za kumeta-meta;