40. Lakini yule wa pili akamjibu akamkemea, akisema, Wewe humwogopi hata Mungu, nawe u katika hukumu iyo hiyo?
41. Nayo ni haki kwetu sisi, kwa kuwa tunapokea malipo tuliyostahili kwa matendo yetu; bali huyu hakutenda lo lote lisilofaa.
42. Kisha akasema, Ee Yesu, nikumbuke utakapoingia katika ufalme wako.
43. Yesu akamwambia, Amin, nakuambia, leo hivi utakuwa pamoja nami peponi.
44. Hapo ilikuwa yapata saa sita, kukawa giza juu ya nchi yote hata saa kenda,
45. jua limepungua nuru yake; pazia la hekalu likapasuka katikati.
46. Yesu akalia kwa sauti kuu, akasema, Ee Baba, mikononi mwako naiweka roho yangu.
47. Alipokwisha kusema hayo alikata roho. Yule akida alipoona yaliyotukia, alimtukuza Mungu, akisema, Hakika yake, mtu huyu alikuwa mwenye haki.