24. Pilato akahukumu kwamba haja yao ifanyike.
25. Akamfungua yule aliyetupwa gerezani kwa ajili ya fitina na uuaji, yule waliyemtaka, akamtoa Yesu wamfanyie watakavyo.
26. Na walipokuwa wakimwondoa walimkamata mtu mmoja, Simoni Mkirene, aliyekuwa ametoka shamba, wakamtwika msalaba, auchukue nyuma yake Yesu.
27. Mkutano mkubwa wa watu wakamfuata, na wanawake waliokuwa wakijipiga vifua na kumwombolezea.
28. Yesu akawageukia, akasema, Enyi binti za Yerusalemu, msinililie mimi, bali jililieni nafsi zenu na watoto wenu.
29. Kwa maana tazama, siku zitakuja watakaposema, Heri walio tasa, na matumbo yasiyozaa, na maziwa yasiyonyonyesha.
30. Ndipo watakapoanza kuiambia milima, Tuangukieni, na vilima, Tufunikeni.
31. Kwa kuwa kama wakitenda mambo haya katika mti mbichi, itakuwaje katika mkavu?
32. Wakapelekwa na wawili wengine, wahalifu, wauawe pamoja naye.