Lk. 23:20-26 Swahili Union Version (SUV)

20. Basi Pilato alisema nao mara ya pili, kwa vile alivyotaka kumfungua Yesu.

21. Lakini wakapiga kelele, wakisema, Msulibishe. Msulibishe.

22. Akawaambia mara ya tatu, Kwa sababu gani? Huyu ametenda uovu gani? Sikuona kwake hata neno lipasalo kufa. Basi nikiisha kumrudi nitamfungua.

23. Lakini wakatoa sauti zao kwa nguvu sana, wakitaka asulibiwe. Sauti zao zikashinda.

24. Pilato akahukumu kwamba haja yao ifanyike.

25. Akamfungua yule aliyetupwa gerezani kwa ajili ya fitina na uuaji, yule waliyemtaka, akamtoa Yesu wamfanyie watakavyo.

26. Na walipokuwa wakimwondoa walimkamata mtu mmoja, Simoni Mkirene, aliyekuwa ametoka shamba, wakamtwika msalaba, auchukue nyuma yake Yesu.

Lk. 23