14. akawaambia, Mtu huyu mmemleta kwangu kana kwamba anapotosha watu; nami, tazama, nimeamua mambo yake mbele yenu, ila sikuona kwake kosa lo lote katika mambo hayo mliyomshitaki;
15. wala hata Herode, kwa maana amemrudisha kwetu; basi tazama, hakuna neno lo lote alilolitenda lipasalo kufa.
16. Kwa hiyo nitamrudi, kisha nitamfungua. [
17. Maana ilimlazimu kuwafungulia mfungwa mmoja wakati wa sikukuu.]