Lk. 23:14-17 Swahili Union Version (SUV)

14. akawaambia, Mtu huyu mmemleta kwangu kana kwamba anapotosha watu; nami, tazama, nimeamua mambo yake mbele yenu, ila sikuona kwake kosa lo lote katika mambo hayo mliyomshitaki;

15. wala hata Herode, kwa maana amemrudisha kwetu; basi tazama, hakuna neno lo lote alilolitenda lipasalo kufa.

16. Kwa hiyo nitamrudi, kisha nitamfungua. [

17. Maana ilimlazimu kuwafungulia mfungwa mmoja wakati wa sikukuu.]

Lk. 23