12. Basi siku ile ile Herode na Pilato walipatana kwa urafiki kwa maana hapo kwanza walikuwa na uadui wao kwa wao.
13. Na Pilato akawakutanisha wakuu wa makuhani, na wakubwa, na watu,
14. akawaambia, Mtu huyu mmemleta kwangu kana kwamba anapotosha watu; nami, tazama, nimeamua mambo yake mbele yenu, ila sikuona kwake kosa lo lote katika mambo hayo mliyomshitaki;
15. wala hata Herode, kwa maana amemrudisha kwetu; basi tazama, hakuna neno lo lote alilolitenda lipasalo kufa.
16. Kwa hiyo nitamrudi, kisha nitamfungua. [
17. Maana ilimlazimu kuwafungulia mfungwa mmoja wakati wa sikukuu.]
18. Wakapiga kelele wote pamoja, wakisema, Mwondoe huyu, utufungulie Baraba.
19. Naye ni mtu aliyetupwa gerezani kwa ajili ya fitina iliyotokea mjini, na kwa uuaji
20. Basi Pilato alisema nao mara ya pili, kwa vile alivyotaka kumfungua Yesu.
21. Lakini wakapiga kelele, wakisema, Msulibishe. Msulibishe.
22. Akawaambia mara ya tatu, Kwa sababu gani? Huyu ametenda uovu gani? Sikuona kwake hata neno lipasalo kufa. Basi nikiisha kumrudi nitamfungua.
23. Lakini wakatoa sauti zao kwa nguvu sana, wakitaka asulibiwe. Sauti zao zikashinda.