12. Basi siku ile ile Herode na Pilato walipatana kwa urafiki kwa maana hapo kwanza walikuwa na uadui wao kwa wao.
13. Na Pilato akawakutanisha wakuu wa makuhani, na wakubwa, na watu,
14. akawaambia, Mtu huyu mmemleta kwangu kana kwamba anapotosha watu; nami, tazama, nimeamua mambo yake mbele yenu, ila sikuona kwake kosa lo lote katika mambo hayo mliyomshitaki;
15. wala hata Herode, kwa maana amemrudisha kwetu; basi tazama, hakuna neno lo lote alilolitenda lipasalo kufa.
16. Kwa hiyo nitamrudi, kisha nitamfungua. [
17. Maana ilimlazimu kuwafungulia mfungwa mmoja wakati wa sikukuu.]
18. Wakapiga kelele wote pamoja, wakisema, Mwondoe huyu, utufungulie Baraba.