Lk. 22:14-22 Swahili Union Version (SUV)

14. Hata saa ilipofika aliketi chakulani, yeye na wale mitume pamoja naye.

15. Akawaambia, Nimetamani sana kuila pasaka hii pamoja nanyi kabla ya kuteswa kwangu;

16. kwa maana nawaambia ya kwamba siili tena hata itakapotimizwa katika ufalme wa Mungu.

17. Akapokea kikombe, akashukuru, akasema, Twaeni hiki, mgawanye ninyi kwa ninyi;

18. Maana nawaambia ya kwamba tangu sasa sinywi mazao ya mzabibu hata ufalme wa Mungu utakapokuja.

19. Akatwaa mkate, akashukuru, akaumega, akawapa, akisema, [Huu ndio mwili wangu unaotolewa kwa ajili yenu; fanyeni hivi kwa ukumbusho wangu.

20. Kikombe nacho vivyo hivyo baada ya kula; akisema, Kikombe hiki ni agano jipya katika damu yangu, inayomwagika kwa ajili yenu.]

21. Walakini, tazama, mkono wake yeye anayenisaliti upo hapa pamoja nami mezani,

22. Kwa kuwa Mwana wa Adamu aenda zake kama ilivyokusudiwa; lakini, ole wake mtu yule amsalitiye!

Lk. 22