Lk. 22:12-18 Swahili Union Version (SUV)

12. Naye atawaonyesha chumba kikubwa orofani, kimekwisha andikwa; andaeni humo.

13. Wakaenda, wakaona kama alivyowaambia, wakaiandaa pasaka.

14. Hata saa ilipofika aliketi chakulani, yeye na wale mitume pamoja naye.

15. Akawaambia, Nimetamani sana kuila pasaka hii pamoja nanyi kabla ya kuteswa kwangu;

16. kwa maana nawaambia ya kwamba siili tena hata itakapotimizwa katika ufalme wa Mungu.

17. Akapokea kikombe, akashukuru, akasema, Twaeni hiki, mgawanye ninyi kwa ninyi;

18. Maana nawaambia ya kwamba tangu sasa sinywi mazao ya mzabibu hata ufalme wa Mungu utakapokuja.

Lk. 22