Lk. 22:11-16 Swahili Union Version (SUV)

11. Na mtamwambia mwenye nyumba, Mwalimu akuambia, Ki wapi chumba cha wageni, nipate kula pasaka humo pamoja na wanafunzi wangu?

12. Naye atawaonyesha chumba kikubwa orofani, kimekwisha andikwa; andaeni humo.

13. Wakaenda, wakaona kama alivyowaambia, wakaiandaa pasaka.

14. Hata saa ilipofika aliketi chakulani, yeye na wale mitume pamoja naye.

15. Akawaambia, Nimetamani sana kuila pasaka hii pamoja nanyi kabla ya kuteswa kwangu;

16. kwa maana nawaambia ya kwamba siili tena hata itakapotimizwa katika ufalme wa Mungu.

Lk. 22