13. Na hayo yatakuwa ushuhuda kwenu.
14. Basi, kusudieni mioyoni mwenu, kutofikiri-fikiri kwanza mtakavyojibu;
15. kwa sababu mimi nitawapa kinywa na hekima ambayo watesi wenu wote hawataweza kushindana nayo wala kuipinga.
16. Nanyi mtasalitiwa na wazazi wenu, na ndugu zenu, na jamaa zenu, na rafiki zenu, nao watawafisha baadhi yenu.
17. Nanyi mtachukiwa na watu wote kwa ajili ya jina langu.
18. Walakini hautapotea hata unywele mmoja wa vichwa vyenu.