38. Naye si Mungu wa wafu, bali wa walio hai; kwa kuwa wote huishi kwake.
39. Waandishi wengine wakajibu wakamwambia, Mwalimu, umesema vema;
40. wala hawakuthubutu kumwuliza neno baada ya hayo.
41. Akawaambia, Wasemaje watu kwamba Kristo ni Mwana wa Daudi?
42. Maana, Daudi mwenyewe asema katika chuo cha Zaburi,Bwana alimwambia Bwana wangu,Uketi mkono wangu wa kuume,