Lk. 20:32-38 Swahili Union Version (SUV)

32. Mwisho akafa yule mke naye.

33. Basi, katika ufufuo atakuwa mke wa yupi? Maana aliolewa na wote saba.

34. Yesu akawaambia, Wana wa ulimwengu huu huoa na kuolewa;

35. lakini, wale wahesabiwao kuwa wamestahili kuupata ulimwengu ule, na kule kufufuka katika wafu, hawaoi wala hawaolewi;

36. wala hawawezi kufa tena; kwa sababu huwa sawasawa na malaika, nao ni wana wa Mungu, kwa vile walivyo wana wa ufufuo.

37. Lakini, ya kuwa wafu hufufuliwa, hata na Musa alionyesha katika sura ya Kijiti, hapo alipomtaja Bwana kuwa ni Mungu wa Ibrahimu, na Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo.

38. Naye si Mungu wa wafu, bali wa walio hai; kwa kuwa wote huishi kwake.

Lk. 20