Lk. 20:1-5 Swahili Union Version (SUV)

1. Ikawa siku moja, alipokuwa akiwafundisha watu hekaluni, na kuihubiri habari njema, wakuu wa makuhani na waandishi pamoja na wazee walimtokea ghafula;

2. wakamwambia, wakisema, Tuambie, unatenda mambo hayo kwa mamlaka gani? Tena, ni nani aliyekupa mamlaka hii?

3. Akajibu akawaambia, Nami nitawauliza ninyi neno moja; niambieni,

4. Ubatizo wa Yohana, je! Ulitoka mbinguni au kwa wanadamu?

5. Wakahojiana wao kwa wao, wakisema, Kama tukisema ulitoka mbinguni, atasema, Basi, mbona hamkumwamini?

Lk. 20