29. Sasa, Bwana, wamruhusu mtumishi wako,Kwa amani, kama ulivyosema;
30. Kwa kuwa macho yangu yameuona wokovu wako,
31. Uliouweka tayari machoni pa watu wote;
32. Nuru ya kuwa mwangaza wa Mataifa,Na kuwa utukufu wa watu wako Israeli.
33. Na babaye na mamaye walikuwa wakiyastaajabia hayo yaliyonenwa juu yake.