Lk. 2:28-35 Swahili Union Version (SUV)

28. yeye mwenyewe alimpokea mikononi mwake, akamshukuru Mungu, akisema,

29. Sasa, Bwana, wamruhusu mtumishi wako,Kwa amani, kama ulivyosema;

30. Kwa kuwa macho yangu yameuona wokovu wako,

31. Uliouweka tayari machoni pa watu wote;

32. Nuru ya kuwa mwangaza wa Mataifa,Na kuwa utukufu wa watu wako Israeli.

33. Na babaye na mamaye walikuwa wakiyastaajabia hayo yaliyonenwa juu yake.

34. Simeoni akawabariki, akamwambia Mariamu mama yake, Tazama, huyu amewekwa kwa kuanguka na kuinuka wengi walio katika Israeli, na kuwa ishara itakayonenewa.

35. Nawe mwenyewe, upanga utaingia moyoni mwako, ili yafunuliwe mawazo ya mioyo mingi.

Lk. 2