17. Walipomwona wakatoa habari waliyoambiwa juu ya huyo mtoto.
18. Wote waliosikia wakastaajabu kwa hayo waliyoambiwa na wachungaji.
19. Lakini Mariamu akayaweka maneno hayo yote, akiyafikiri moyoni mwake.
20. Wale wachungaji wakarudi, huku wanamtukuza Mungu na kumsifu kwa mambo yote waliyosikia na kuyaona, kama walivyoambiwa.
21. Hata zilipotumia siku nane za kumtahiri, aliitwa jina lake Yesu; kama alivyoitwa na malaika kabla hajachukuliwa mimba.