Lk. 19:31-35 Swahili Union Version (SUV)

31. Na kama mtu akiwauliza, Mbona mnamfungua? Semeni hivi, Bwana anamhitaji.

32. Na wale waliotumwa wakaenda wakaona kama alivyowaambia.

33. Na walipokuwa wakimfungua mwana-punda, wenyewe waliwaambia, Mbona mnamfungua mwana-punda?

34. Wakasema, Bwana ana haja naye.

35. Wakampeleka kwa Yesu, wakatandika nguo zao juu ya mwana-punda, wakampandisha Yesu.

Lk. 19