Lk. 19:27-30 Swahili Union Version (SUV)

27. Tena, wale adui zangu, wasiotaka niwatawale, waleteni hapa mwachinje mbele yangu.

28. Na alipokwisha kusema hayo, alitangulia mbele akipanda kwenda Yerusalemu.

29. Ikawa alipokaribia Bethfage na Bethania, kwenye mlima uitwao wa Mizeituni, alituma wawili katika wale wanafunzi,

30. akisema, Nendeni mpaka kijiji kile kinachowakabili, na mtakapoingia ndani mtaona mwana-punda, amefungwa, ambaye hajapandwa na mtu ye yote bado, mfungueni mkamlete hapa.

Lk. 19