Lk. 18:36-41 Swahili Union Version (SUV)

36. na alipowasikia makutano wakipita, aliuliza, Kuna nini?

37. Wakamwambia, Yesu wa Nazareti anapita.

38. Akapiga kelele, akisema, Yesu, Mwana wa Daudi, unirehemu.

39. Basi wale waliotangulia wakamkemea ili anyamaze; lakini yeye alizidi sana kupaza sauti, Ee Mwana wa Daudi, unirehemu.

40. Yesu akasimama, akaamuru aletwe kwake; na alipomkaribia, alimwuliza,

41. Wataka nikufanyie nini? Akasema, Bwana, nipate kuona.

Lk. 18