34. Walakini hawakuelewa maneno hayo hata kidogo, na jambo hilo lilikuwa limefichwa kwao, wala hawakufahamu yaliyonenwa.
35. Ikawa alipokaribia Yeriko, mtu mmoja kipofu alikuwa ameketi kando ya njia, akiomba sadaka;
36. na alipowasikia makutano wakipita, aliuliza, Kuna nini?
37. Wakamwambia, Yesu wa Nazareti anapita.
38. Akapiga kelele, akisema, Yesu, Mwana wa Daudi, unirehemu.
39. Basi wale waliotangulia wakamkemea ili anyamaze; lakini yeye alizidi sana kupaza sauti, Ee Mwana wa Daudi, unirehemu.
40. Yesu akasimama, akaamuru aletwe kwake; na alipomkaribia, alimwuliza,
41. Wataka nikufanyie nini? Akasema, Bwana, nipate kuona.
42. Yesu akamwambia, Upewe kuona; imani yako imekuponya.
43. Mara hiyo akapata kuona, akamfuata, huku akimtukuza Mungu. Na watu wote walipoona hayo walimsifu Mungu.