Lk. 18:31-33 Swahili Union Version (SUV)

31. Akawachukua wale Thenashara, akawaambia, Tazameni, tunapanda kwenda Yerusalemu, na mambo yote yatatimizwa, Mwana wa Adamu aliyoandikiwa na manabii.

32. Kwa kuwa atatiwa mikononi mwa Mataifa, atafanyiwa dhihaka; atatendwa jeuri, na kutemewa mate;

33. nao watampiga mijeledi, kisha watamwua; na siku ya tatu atafufuka.

Lk. 18