Lk. 18:23-27 Swahili Union Version (SUV)

23. Lakini aliposikia hayo alihuzunika sana, maana alikuwa na mali nyingi.

24. Yesu alipoona vile alisema, Kwa shida gani wenye mali watauingia ufalme wa Mungu!

25. Kwa maana ni vyepesi ngamia kupita katika tundu la sindano kuliko tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu.

26. Nao waliosikia walisema, Ni nani basi awezaye kuokoka?

27. Akasema, Yasiyowezekana kwa wanadamu yawezekana kwa Mungu.

Lk. 18