25. Basi, yule mwanawe mkubwa alikuwako shamba na alipokuwa akija na kuikaribia nyumba, alisikia sauti ya nyimbo na machezo.
26. Akaita mtumishi mmoja, akamwuliza, Mambo haya, maana yake nini?
27. Akamwambia, Ndugu yako amekuja, na baba yako amemchinja ndama aliyenona, kwa sababu amempata tena, yu mzima.
28. Akakasirika, akakataa kuingia ndani. Basi babaye alitoka nje, akamsihi.