Lk. 14:1-7 Swahili Union Version (SUV)

1. Ikawa alipoingia ndani ya nyumba ya mtu mmoja miongoni mwa wakuu wa Mafarisayo siku ya sabato, ale chakula, walikuwa wakimvizia.

2. Na tazama, mbele yake palikuwa na mtu mwenye ugonjwa wa safura.

3. Yesu akajibu, akawaambia wana-sheria na Mafarisayo, Je! Ni halali kuponya siku ya sabato, ama sivyo?

4. Wao wakanyamaza. Akamshika, akamponya, akamruhusu aende zake.

5. Akawaambia, Ni nani miongoni mwenu, ikiwa ng’ombe wake au punda wake ametumbukia kisimani, asiyemwopoa mara hiyo siku ya sabato?

6. Nao hawakuweza kujibu maneno haya.

7. Akawaambia mfano wale walioalikwa, alipoona jinsi walivyochagua viti vya mbele; akisema,

Lk. 14