Lk. 1:69-75 Swahili Union Version (SUV)

69. Ametusimamishia pembe ya wokovuKatika mlango wa Daudi, mtumishi wake.

70. Kama alivyosema tangu mwanzoKwa kinywa cha manabii wake watakatifu;

71. Tuokolewe na adui zetuNa mikononi mwao wote wanaotuchukia;

72. Ili kuwatendea rehema baba zetu,Na kulikumbuka agano lake takatifu;

73. Uapo aliomwapia Ibrahimu, baba yetu,

74. Ya kwamba atatujalia sisi,Tuokoke mikononi mwa adui zetu,Na kumwabudu pasipo hofu,

75. Kwa utakatifu na kwa hakiMbele zake siku zetu zote.

Lk. 1