69. Ametusimamishia pembe ya wokovuKatika mlango wa Daudi, mtumishi wake.
70. Kama alivyosema tangu mwanzoKwa kinywa cha manabii wake watakatifu;
71. Tuokolewe na adui zetuNa mikononi mwao wote wanaotuchukia;
72. Ili kuwatendea rehema baba zetu,Na kulikumbuka agano lake takatifu;
73. Uapo aliomwapia Ibrahimu, baba yetu,
74. Ya kwamba atatujalia sisi,Tuokoke mikononi mwa adui zetu,Na kumwabudu pasipo hofu,
75. Kwa utakatifu na kwa hakiMbele zake siku zetu zote.