59. Ikawa siku ya nane wakaja kumtahiri mtoto; wakataka kumpa jina la babaye, Zakaria.
60. Mamaye akajibu akasema La, sivyo; bali, ataitwa Yohana.
61. Wakamwambia, Hapana mtu katika jamaa zako aitwaye jina hilo.
62. Wakamwashiria babaye wajue atakavyo kumwita.
63. Akataka kibao, akaandika ya kwamba, Jina lake ni Yohana. Wakastaajabu wote.