Lk. 1:59-63 Swahili Union Version (SUV)

59. Ikawa siku ya nane wakaja kumtahiri mtoto; wakataka kumpa jina la babaye, Zakaria.

60. Mamaye akajibu akasema La, sivyo; bali, ataitwa Yohana.

61. Wakamwambia, Hapana mtu katika jamaa zako aitwaye jina hilo.

62. Wakamwashiria babaye wajue atakavyo kumwita.

63. Akataka kibao, akaandika ya kwamba, Jina lake ni Yohana. Wakastaajabu wote.

Lk. 1