46. Mariamu akasema,Moyo wangu wamwadhimisha Bwana,
47. Na roho yangu imemfurahia Mungu, Mwokozi wangu;
48. Kwa kuwa ameutazamaUnyonge wa mjakazi wake.Kwa maana, tazama, tokea sasaVizazi vyote wataniita mbarikiwa;
49. Kwa kuwa Mwenye nguvu amenitendea makuu,Na jina lake ni takatifu.
50. Na rehema zake hudumu vizazi hata vizaziKwa hao wanaomcha.
51. Amefanya nguvu kwa mkono wake;Amewatawanya walio na kiburi katika mawazo ya mioyo yao;
52. Amewaangusha wakuu katika viti vyao vya enzi;Na wanyonge amewakweza.
53. Wenye njaa amewashibisha mema,Na wenye mali amewaondoa mikono mitupu.
54. Amemsaidia Israeli, mtumishi wake;Ili kukumbuka rehema zake;
55. Kama alivyowaambia baba zetu,Ibrahimu na uzao wake hata milele.
56. Mariamu akakaa naye kadiri ya miezi mitatu, kisha akarudi kwenda nyumbani kwake.