44. Maana sauti ya kuamkia kwako ilipoingia masikioni mwangu, kitoto kichanga kikaruka kwa shangwe ndani ya tumbo langu.
45. Naye heri aliyesadiki; kwa maana yatatimizwa aliyoambiwa na Bwana.
46. Mariamu akasema,Moyo wangu wamwadhimisha Bwana,
47. Na roho yangu imemfurahia Mungu, Mwokozi wangu;
48. Kwa kuwa ameutazamaUnyonge wa mjakazi wake.Kwa maana, tazama, tokea sasaVizazi vyote wataniita mbarikiwa;
49. Kwa kuwa Mwenye nguvu amenitendea makuu,Na jina lake ni takatifu.
50. Na rehema zake hudumu vizazi hata vizaziKwa hao wanaomcha.
51. Amefanya nguvu kwa mkono wake;Amewatawanya walio na kiburi katika mawazo ya mioyo yao;
52. Amewaangusha wakuu katika viti vyao vya enzi;Na wanyonge amewakweza.
53. Wenye njaa amewashibisha mema,Na wenye mali amewaondoa mikono mitupu.
54. Amemsaidia Israeli, mtumishi wake;Ili kukumbuka rehema zake;
55. Kama alivyowaambia baba zetu,Ibrahimu na uzao wake hata milele.
56. Mariamu akakaa naye kadiri ya miezi mitatu, kisha akarudi kwenda nyumbani kwake.
57. Ikawa, siku za kuzaa kwake Elisabeti zilipotimia, alizaa mtoto mwanamume.