42. akapaza sauti kwa nguvu akasema, Umebarikiwa wewe katika wanawake, naye mzao wa tumbo lako amebarikiwa.
43. Limenitokeaje neno hili, hata mama wa Bwana wangu anijilie mimi?
44. Maana sauti ya kuamkia kwako ilipoingia masikioni mwangu, kitoto kichanga kikaruka kwa shangwe ndani ya tumbo langu.
45. Naye heri aliyesadiki; kwa maana yatatimizwa aliyoambiwa na Bwana.
46. Mariamu akasema,Moyo wangu wamwadhimisha Bwana,
47. Na roho yangu imemfurahia Mungu, Mwokozi wangu;
48. Kwa kuwa ameutazamaUnyonge wa mjakazi wake.Kwa maana, tazama, tokea sasaVizazi vyote wataniita mbarikiwa;