40. akaingia nyumbani kwa Zakaria akamwamkia Elisabeti.
41. Ikawa Elisabeti aliposikia kule kuamkia kwake Mariamu, kitoto kichanga kikaruka ndani ya tumbo lake; Elisabeti akajazwa Roho Mtakatifu;
42. akapaza sauti kwa nguvu akasema, Umebarikiwa wewe katika wanawake, naye mzao wa tumbo lako amebarikiwa.
43. Limenitokeaje neno hili, hata mama wa Bwana wangu anijilie mimi?
44. Maana sauti ya kuamkia kwako ilipoingia masikioni mwangu, kitoto kichanga kikaruka kwa shangwe ndani ya tumbo langu.
45. Naye heri aliyesadiki; kwa maana yatatimizwa aliyoambiwa na Bwana.
46. Mariamu akasema,Moyo wangu wamwadhimisha Bwana,
47. Na roho yangu imemfurahia Mungu, Mwokozi wangu;
48. Kwa kuwa ameutazamaUnyonge wa mjakazi wake.Kwa maana, tazama, tokea sasaVizazi vyote wataniita mbarikiwa;
49. Kwa kuwa Mwenye nguvu amenitendea makuu,Na jina lake ni takatifu.
50. Na rehema zake hudumu vizazi hata vizaziKwa hao wanaomcha.
51. Amefanya nguvu kwa mkono wake;Amewatawanya walio na kiburi katika mawazo ya mioyo yao;