Law. 8:1-6 Swahili Union Version (SUV)

1. BWANA akanena na Musa, na kumwambia,

2. Mtwae Haruni, na wanawe pamoja naye, na yale mavazi, na mafuta ya kutia, na ng’ombe mume wa sadaka ya dhambi, na kondoo waume wawili, na kikapu cha mikate isiyotiwa chachu;

3. kisha ukutanishe mkutano wote hapo mlangoni pa hema ya kukutania.

4. Basi Musa akafanya kama alivyoambiwa na BWANA; na huo mkutano ulikutanishwa mlangoni pa hema ya kukutania.

5. Musa akawaambia mkutano, Neno aliloliagiza BWANA kwamba lifanywe, ni hili.

6. Basi Musa akawaleta Haruni na wanawe, akawaosha kwa maji.

Law. 8