Law. 24:18-22 Swahili Union Version (SUV)

18. na atakayempiga mnyama hata akafa atalipa; uhai kwa uhai.

19. Na mtu akimtia mwenziwe kilema; vile vile kama alivyofanya, naye atafanyiwa vivyo;

20. jeraha kwa jeraha, jicho kwa jicho, jino kwa jino; vile vile kama alivyomtia mtu kilema, naye atalipwa vivyo.

21. Na mtu amwuaye mnyama atalipa; na yeye atakayemwua binadamu atauawa.

22. Mtakuwa na sheria moja tu, kwa huyo aliye mgeni, na kwa mzalia; kwa kuwa mimi ndimi BWANA, Mungu wenu.

Law. 24