18. na atakayempiga mnyama hata akafa atalipa; uhai kwa uhai.
19. Na mtu akimtia mwenziwe kilema; vile vile kama alivyofanya, naye atafanyiwa vivyo;
20. jeraha kwa jeraha, jicho kwa jicho, jino kwa jino; vile vile kama alivyomtia mtu kilema, naye atalipwa vivyo.
21. Na mtu amwuaye mnyama atalipa; na yeye atakayemwua binadamu atauawa.
22. Mtakuwa na sheria moja tu, kwa huyo aliye mgeni, na kwa mzalia; kwa kuwa mimi ndimi BWANA, Mungu wenu.