Law. 19:24-29 Swahili Union Version (SUV)

24. Lakini mwaka wa nne matunda yake yote yatakuwa ni matakatifu, kwa ajili ya kumpa BWANA shukrani.

25. Na katika mwaka wa tano mtakula katika matunda yake, ili ipate kuwapa maongeo yake; mimi ndimi BWANA, Mungu wenu.

26. Msile kitu cho chote pamoja na damu yake; wala msifanye kuloga, wala kutumia utambuzi.

27. Msinyoe denge pembe za vichwani, wala msiharibu pembe za ndevu zenu.

28. Msichanje chale yo yote katika nyama ya miili yenu kwa ajili ya wafu, wala msiandike alama miilini mwenu; mimi ndimi BWANA.

29. Usimnajisi binti yako, ili kumfanya awe kahaba; isiwe hiyo nchi kuuandama ukahaba, na nchi kujawa na uovu mkuu.

Law. 19