Law. 18:12-18 Swahili Union Version (SUV)

12. Usifunue utupu wa umbu lake baba yako; maana, yeye ni jamaa aliye karibu.

13. Usifunue utupu wa umbu la mama yako; maana, yeye ni jamaa ya mama yako ya karibu.

14. Usifunue utupu wa ndugu ya baba yako, usimkaribie mkewe huyo; yeye ni shangazi lako.

15. Usifunue utupu wa mkweo mwanamke; yeye ni mke wa mwanao; usifunue utupu wake huyo.

16. Usifunue utupu wa mke wa nduguyo; maana, ni utupu wa nduguyo.

17. Usifunue utupu wa mwanamke na binti yake; usimtwae binti ya mwanawe mume, au binti ya binti yake, ili kufunua utupu wake; hao ni jamaa ya karibu; ni uovu mkuu.

18. Wala usitwae mwanamke pamoja na nduguye, awe mtesi wake, na kufunua utupu wake, huyo wa pili atakapokuwa yu hai.

Law. 18