Law. 14:52-57 Swahili Union Version (SUV)

52. naye ataitakasa hiyo nyumba kwa damu ya ndege, na kwa maji ya mtoni, na kwa huyo ndege aliye hai, na kwa mti wa mwerezi, na kwa hisopo, na kwa sufu nyekundu;

53. lakini ndege aliye hai atamwacha atoke mle mjini aende nyikani; ndivyo atakavyofanya upatanisho kwa ajili ya hiyo nyumba; nayo itakuwa safi.

54. Hiyo ndiyo sheria ya pigo la ukoma ya kila aina, na ya kipwepwe;

55. na ya ukoma wa vazi, na ukoma wa nyumba;

56. na kivimbe, na kikoko na kipaku king’aacho;

57. ili kufunza itakapokuwa ni unajisi, na itakapokuwa ni safi; hiyo ndiyo sheria ya ukoma.

Law. 14