16. na mbuni, na kirukanjia, na dudumizi, na kipanga kwa aina zake;
17. na bundi, na mnandi, na bundi mkubwa;
18. na mumbi, na mwari, na mderi;
19. na korongo, na koikoi kwa aina zake, na hudihudi, na popo.
20. Tena vyote vitambaavyo vyenye mabawa viendavyo kwa miguu minne, hivi ni machukizo kwenu.
21. Pamoja na hayo, hivi vitambaavyo vyenye mabawa viendavyo kwa miguu minne ni halali kula, hao walio na miguu mirefu, ya kurukia juu ya nchi;