Law. 11:13-18 Swahili Union Version (SUV)

13. Kisha katika ndege hawa watakuwa ni machukizo kwenu; hawataliwa, ndio machukizo; tai, na furukombe, na kipungu;

14. na mwewe, na kozi kwa aina zake,

15. na kila kunguru kwa aina zake;

16. na mbuni, na kirukanjia, na dudumizi, na kipanga kwa aina zake;

17. na bundi, na mnandi, na bundi mkubwa;

18. na mumbi, na mwari, na mderi;

Law. 11