12. Kila asiye na mapezi wala magamba aliye ndani ya maji ni machukizo kwenu.
13. Kisha katika ndege hawa watakuwa ni machukizo kwenu; hawataliwa, ndio machukizo; tai, na furukombe, na kipungu;
14. na mwewe, na kozi kwa aina zake,
15. na kila kunguru kwa aina zake;
16. na mbuni, na kirukanjia, na dudumizi, na kipanga kwa aina zake;