Kut. 7:11-14 Swahili Union Version (SUV)

11. Ndipo Farao naye akawaita wenye akili na wachawi; na hao waganga wa Misri wakafanya vivyo kwa uganga wao.

12. Wakabwaga chini kila mtu fimbo yake, nazo zikawa nyoka; lakini fimbo ya Haruni ikazimeza fimbo zao.

13. Moyo wa Farao ukawa ni mgumu asiwasikize; kama BWANA alivyonena.

14. BWANA akamwambia Musa, Moyo wa Farao ni mzito, anakataa kuwapa watu ruhusa waende zao.

Kut. 7