Kut. 6:27-30 Swahili Union Version (SUV)

27. Ni hao walionena na Farao mfalme wa Misri ili wawatoe wana wa Israeli watoke Misri; hao ni Musa ye yule, na Haruni ye yule.

28. Ilikuwa siku hiyo BWANA aliponena na Musa katika nchi ya Misri,

29. BWANA akamwambia Musa, akasema, Mimi ni BWANA; mwambie Farao mfalme wa Misri maneno yote nikuambiayo.

30. Musa akanena mbele ya BWANA, Mimi ni mtu mwenye midomo isiyo tohara, Farao atanisikizaje?

Kut. 6