21. BWANA akasema, Tazama, hapa pana mahali karibu nami, nawe utasimama juu ya mwamba;
22. kisha itakuwa wakati unapopita utukufu wangu, nitakutia katika ufa wa ule mwamba, na kukufunika kwa mkono wangu hata nitakapokuwa nimekwisha kupita;
23. nami nitaondoa mkono wangu, nawe utaniona nyuma yangu, bali uso wangu hautaonekana.